Elon Musk Kuzindua Mpinzani Wa Mtandao wa WhatsApp Unaitwa XCHAT

-rickmedia: Lanka Ting

Lanka Ting

2 days ago
rickmedia: elon-musk-kuzindua-mpinzani-mtandao-whatsapp-unaitwa-xchat-878-rickmedia

Tajiri wa teknolojia #ElonMusk amethibitisha kuwa atazindua Mtandao wake wa #XChat, jukwaa la ujumbe linalodhaniwa kuwa mshindani wa #WhatsApp.

Kwa mujibu wa Musk, XChat inatarajiwa kuanza kutolewa wakati wowote, ikiwa na kipengele cha kipekee cha uwezo wa kutuma na/au kupokea simu za sauti au video bila namba ya simu.

Vipengele vingine ni pamoja na ujumbe unaopotea baada ya muda na uwezo wa kutuma “aina yoyote ya faili.”

Ingawa programu hiyo bado haijapatikana rasmi, baadhi ya watumiaji wa X wanaolipia huduma ya premium ya jukwaa hilo (inaripotiwa) tayari wameweza kupata huduma ya XChat.