Donald Trump amesema kuwa China inaweza kuendelea kununua mafuta ya Iran

-rickmedia: Lanka Ting

Lanka Ting

8 hours ago
rickmedia: donald-trump-amesema-kuwa-china-inaweza-kuendelea-kununua-mafuta-iran-892-rickmedia

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa China inaweza kuendelea kununua mafuta ya Iran baada ya Israel na Iran kukubaliana kusitisha mapigano,hatua ambayo Ikulu ya White House ilifafanua kuwa ni kulegeza vikwazo vya Marekani.

"china sasa inaweza kuendelea kununua Mafuta kutoka Iran. Tunatumai, watakuwa wakinunua mafuta mengi kutoka Marekani pia," Trump alisema kwenye chapisho kwenye Truth Social, siku chache tu baada ya kuamuru Marekani kulipuliwa maeneo matatu ya nyuklia ya Iran.

Trump alikuwa akizingatia uamuzi wa Iran wa kutofunga Mlango-Bahari wa Hormuz kwa meli za mafuta, hatua ambayo ingekuwa ngumu kwa China, muagizaji mkuu wa kimataifa wa mafuta ya Irani, afisa mkuu wa Ikulu ya White aliambia Reuters.

"Rais anaendelea kutoa wito kwa China na nchi zote kuagiza mafuta yetu ya kisasa zaidi kuliko kuagiza mafuta ya Iran kinyume na vikwazo vya Marekani," afisa huyo alisema.

Baada ya tangazo la kusitisha mapigano, maoni ya Trump juu ya china yalikuwa ishara nyingine ya bei ya mafuta, ambayo ilishuka kwa karibu 6%.

Kulegezwa kokote kwa utekelezaji wa vikwazo kwa Iran kutaashiria mabadiliko ya sera za Marekani baada ya Trump kusema mwezi Februari kwamba alikuwa akiiwekea tena shinikizo la juu zaidi Iran, akilenga kusukuma mauzo yake ya mafuta hadi sifuri, kutokana na mpango wake wa nyuklia na ufadhili wa wanamgambo kote Mashariki ya Kati.