Achraf Hakimi ashinda tuzo ya mchezaji bora 2025 Africa, tuzo za CAF

-rickmedia: Saraphina Jerry

Saraphina Jerry

7 hours ago
rickmedia: achraf-hakimi-ashinda-tuzo-mchezaji-bora-2025-africa-tuzo-caf-898-rickmedia

Beki wa Morocco anayeitumikia PSG ya Ufaransa, Achraf Hakimi, ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora Afrika wa CAF 2025.

Katika hafla za utoaji wa tuzo hizo leo, Rabat, Morocco, Hakimi ametangazwa mshindi akiwapiku Mohamed Salah wa Liverpool na Misri pamoja na Victor Osimhen wa Nigeria na Galatasaray.

Katika mwaka huu, Hakimi ameshinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Ligi Kuu Ufaransa, Kombe la Ufaransa na ameiongoza Morocco kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2026.

Kwa upande wa Wanawake, Mchezaji Bora Afrika 2025 ni Ghizlane Chebbak wa Morocco na Klabu ya Al Hilal.