Peter Okoye, aliyekuwa mwanachama wa kundi la muziki la P-Square, amewatuhumu kaka zake, Paul na Jude kwa kujaribu kuharibu jina lake wakati wakikabiliana na kesi ya kisheria inayoendelea.
Wakili wa Jude alidai mahakamani kuwa Peter alitoa taarifa ya uongo kwa Tume ya Kupambana na Rushwa na Uhalifu wa Kiuchumi (EFCC) kuhusu masuala ya malipo ya mrabaha, madai yanayohusiana na mapato ya kazi zao za muziki.