Serikali ya Kenya imethibitisha uwepo wa homa ya Chikungunya katika Kaunti ya Mombasa ambapo watu 25 wamethibitika kuambukizwa.
Kitengo cha Oparesheni za Dharura ya Afya ya Umma kimetangaza dalili za ugonjwa huo kuwa ni pamoja na harara, kujikuna na maumivu makali. Hata hivyo, ugonjwa huo bado hauna matibabu maalum.