Waziri Mkuu Ajiuzulu Kisa Bata la Mtoto wake

-rickmedia: Lanka Ting

Lanka Ting

1 day ago
rickmedia: waziri-mkuu-ajiuzulu-kisa-bata-mtoto-wake-936-rickmedia

Waziri Mkuu wa Mongolia, Oyun-Erdene, amejiuzulu kufuatia maandamano makubwa yaliyozuka baada ya mtindo wa maisha ya kifahari wa mwanawe kuonekana kwenye mitandao ya kijamii.

Mwanawe alionyesha begi la #Dior na mifuko kadhaa ya manunuzi alipokuwa kwenye likizo ya uchumba.

Picha ya begi la #Dior, inaripotiwa kupostiwa na mchumba wake, ilikuwa na maelezo yaliyosomeka: “Happy birthday to me” (Heri ya siku yangu ya kuzaliwa). Picha nyingine ilionyesha wanandoa hao wakibusiana wakiwa katika swimming pool.

Luvsannamsrain Oyun-Erdene, ambaye amekana kufanya kosa lolote, alipoteza kura ya imani bungeni siku ya Jumanne.