Aliebakwa Na Baba Yake Alipwa Milioni 49 Na Kuombwa Msamaha na Polisi

-rickmedia: Lanka Ting

Lanka Ting

4 months ago
rickmedia: aliebakwa-baba-yake-alipwa-milioni-kuombwa-msamaha-polisi-669-rickmedia

Mwanamke ambaye alilawitiwa na baba yake ameshinda kesi na kupokea msamaha kutoka kwa polisi baada ya maafisa kumwambia angeonekana kama mtu mbaya kama atamripoti kwa mamlaka.

#CarolHiggins, 55, alinyanyaswa kingono na baba yake, #ElliotAppleyard, ambaye sasa ana umri wa miaka 76, alipokuwa na umri wa miaka 13.

Mama huyo wa watoto wawili alimripoti #Appleyard kwa polisi mwaka wa 1985, na matukio mengine manne tofauti kuanzia 1984 hadi 2015. Lakini haikuwa hadi 2019 ambapo alifungwa jela miaka 20 kwa uhalifu wake.

Mnamo 1985, #BiHiggins alisema aliambiwa na polisi kuwa jina lake litachafuliwa na kuonekana mtu mbaya kama atamfungulia mashtaka Baba yake.

Alifungua kesi katika mahakama ya kiraia dhidi ya Polisi wa West Yorkshire miaka minne iliyopita - kutokana na jinsi kesi yake ilivyoshughulikiwa kati ya 2005 na 2019.

Kikosi hicho sasa kimeomba radhi kwa kuchukua muda mrefu kumfikisha #Appleyard mahakamani na kumlipa #BiHiggins fidia ya pauni 15,000 (Tsh.Milioni 49).

Hatimaye polisi waliomba msamaha kwa "kuchukua muda mrefu" kuleta "madai mazito na ya kweli" ya Carol mnamo Desemba 2023.

Carol, mwandishi kutoka Penistone, Barnsley, alisema: 'Msamaha ulihisi kama kitulizo kikubwa, na uzito kutoka mabegani baada ya kupambana na polisi kwa muda wote huu.

‘Nina furaha wanajifanya kuwajibika kwa jinsi walivyonitendea. Ilikuwa ni jambo kubwa, kuwa na uthibitisho.