Kocha wa zamani wa Senegal 'Aliou Cisse' ateuliwa Kocha mkuu Angola

-rickmedia: Saraphina Jerry

Saraphina Jerry

1 hour ago
rickmedia: kocha-zamani-senegal-aliou-cisse-ateuliwa-kocha-mkuu-angola-476-rickmedia

Shirikisho la kandanda la Angola limesema leo hii Alhamisi kuwa limemwajiri mshindi wa Kombe la Mataifa ya Afrika kutoka Senegal Aliou Cisse kama kocha mkuu mpya wa timu ya taifa.

Cisse, beki wa zamani wa kimataifa ambaye alikuwa nahodha wa Lions of Teranga ya Senegal hadi robo fainali ya Kombe la Dunia la 2002, alijiuzulu kama kocha wa Libya Jumatano baada ya mechi 10 pekee za kuinoa timu hiyo.

“Leo ni siku ya upya, siku ambayo tunafufua matumaini na kuthibitisha tena kwa imani nia yetu ya mustakabali wa soka la kitaifa,” rais wa Shirikisho la Soka la Angola, Alves Simoes, alisema katika hafla ya kumtambulisha Cisse katika mji mkuu, Luanda.

Kocha huyu mwenye umri wa miaka 50 amesaini mkataba wa miaka minne.