Baada ya Taarifa njema kutoka kwa Staa wa Muzik #DiamondPlatnumz kuwa Amefunga Ndoa na Mpenzi wake ambae pia ni Msanii ambae yupo chini ya Lebo yake ya WCB, #Zuchu, Staa #Harmonize Ameibuka na kuonesha kutokukubaliana na Ndoa hiyo akidai kuwa Sababu ya Diamond kumuoa Zuchu ni kuhakikisha hatoki kwenye Levo yake.
Siku ya jana #Diamond Aliweka wazi kuwa Aliwahi kufunga Ndoa na Zuchu ikisimamiwa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, #WalidAlhad.
Kupitia ukurasa wa Instagram (Instastory), #Harmonize Ameshare picha ya Rapa #Diddy kisha kuisindikiza na ujumbe akidai kuwa #Diamond Amejifanya kumuoa #Zuchu ili tu ashindwe kutoka ndani ya #WCB.