Loading...

Rapa LL Cool J athibitisha kuwepo kwa kolabo yake na Michael Jackson

-rickmedia: Saraphina Jerry

Saraphina Jerry

5 days ago
rickmedia: rapa-cool-athibitisha-kuwepo-kwa-kolabo-yake-michael-jackson-544-rickmedia

Rapa na muigizaji LL Cool J, mwenye umri wa miaka 56, amerudi na albamu yake mpya baada ya zaidi ya. miaka 10. Akihojiwa na Variety, LL Cool J alielezea nia yake ya kubadili mtazamo wa hip-hop kuhusu umri, akisema kuwa watu hawakumuelewa alipoeleza kuwa anataka kurekodi albamu ya kisasa. Albamu yake mpya The Force, iliyotayarishwa na Q-Tip, ni ya kwanza tangu Authentic ya 2013.

LL Cool J alieleza kwamba muziki wake unalenga kudhihirisha kuwa wasanii wakongwe bado wanaweza kuwa na umuhimu kwenye hip-hop, ambayo mara nyingi inaonekana kuwa ya vijana.

Katika mahojiano hayo, alifichua pia kuwa ana muziki ambao haujaachiliwa alioufanya na #MichaelJackson, na kwamba Michael alimuonyesha upendo na heshima kubwa.

"Michael Jackson kwangu ni mfalme," alisema #LLCoolJ, akieleza kuwa bado ni shabiki mkubwa wa mwimbaji huyo maarufu.