Diddy Aomba Dhamana Tena Ya Bilioni 128+

-rickmedia: Lanka Ting

Lanka Ting

7 months ago
rickmedia: diddy-aomba-dhamana-tena-bilioni-128-546-rickmedia

Timu ya mawakili wa rapa na mfanyabiashara #Diddy imewasilisha ombi jipya la dhamana, ikipendekeza bondi ya dola milioni 50, ikihakikishwa kwa jumba lake la kifahari la Miami lenye thamani ya dola milioni 48.

Wanasema #Diddy ndiye pekee aliyeko rumande Marekani kwa kuwaajiri wanaume wa kulipwa kwa mahusiano ya hiari na mpenzi wake, bila ushiriki wa watoto, wakisisitiza kuwa mitazamo ya kijamii imebadilika tangu kupitishwa kwa Sheria ya Mann ya mwaka 1910.

Ombi hilo limewasilishwa kabla ya hukumu yake iliyopangwa Oktoba 3, 2025, ambapo anakabiliwa na mashtaka mawili ya ukahaba. Linadai kuwa kuwekwa kwake rumande ni hatua kali kupita kiasi, na kwamba hana rasilimali za kutosha kujitetea akiwa Kituo cha Metropolitan, Brooklyn.

Waendesha mashtaka wamepinga dhamana hiyo, wakimtaja kuwa ni tishio kwa jamii kutokana na historia ya vurugu, ikiwemo shambulio dhidi ya Cassie Ventura mwaka 2016.