Staa wa Filamu kutoka nchini Marekani Michael B Jordan apata ajali ya gari. Michael amepata ajali hiyo usiku wa Jumamosi ya December 2,2023 akiwa na gari lake aina ya Ferrari.
Kwa mujibu wa TMZ Jordan mwenye miaka 36 alipata ajali na gari lake hilo lenye rangi ya Blue nje ya Studio ya Sunset Gower Studio mida ya saa 11 Alfajiri. Polisi wa Jijini Los Anges wamesema kuwa hawajaona dalili zozote za staa huyo kuwa alikuwa ametumia kilevi mpaka kupelekea Ajali hiyo
Hata hivyo kwa upande wake Michael B Jordan hajatoa sababu ya kupata ajali hiyo.