Mzozo kati ya Israel na Hamas umefikia hatua mbaya kwani zaidi ya watu 10,000 wamefariki Gaza katika muda wa wiki nne tangu mzozo huo uanze.
Mnamo Jumatatu, Novemba 6, Wizara ya Afya huko Gaza iliripoti zaidi ya watu 10,000 wameua na wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto katika vita vilivyoanza karibu mwezi mmoja uliopita baada ya Hamas kushambulia jamii kadhaa za Israeli, na kuua watu 1,400 na kuwateka nyara karibu watu 240.
Zaidi ya wanajeshi 340 wa Israel wamekufa tangu mashambulizi ya Oktoba 7, Israel ilisema.
Mabomu ya Israel yamepiga kambi za wakimbizi. Shambulio moja kwenye kambi ya wakimbizi ya Maghazi mapema Jumapili liliua takriban watu 33 na kujeruhi makumi, maafisa wa afya katika eneo hilo walisema.
Viongozi wa mashirika makubwa ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa pamoja na mashirika ya misaada ya kimataifa wametoa wito wa "kusitishwa mara moja kwa mapigano ya kibinadamu" huko Gaza, na kuitaja hali hiyo kuwa "ya kutisha" na "isiyokubalika" katika taarifa adimu ya pamoja.