Baada ya kufanikiwa kuzunguka kwenye nchi 20 Barani Afrika hatimaye Streamer iShowSpeed amehitimisha ziara yake Barani Afrika.

Ziara hiyo imedumu kwa muda wa siku 28. Kwenye ziara yake hiyo iShowSpeed amefanikiwa kuionesha dunia uhalisia wa bara la Afrika huku akionesha utamaduni na maendeleo makubwa ambayo bara la Afrika limepiga
Ziara hii imewafumbua macho vijana mbalimbali wa Ulaya ambao walikuwa hawafahamu uhalisia wa bara la Afrika. Wapo waliokuwa wanaamini Afrika hakuna maendeleo lakini kupitia ziara hii dunia imejua maendeleo makubwa ambayo bara la Afrika imepiga