Wabunge wamchagua Cyril Ramaphosa kuwa Rais wa Afrika Kusini kwa awamu ya pili

-rickmedia: Saraphina Jerry

Saraphina Jerry

4 months ago
rickmedia: wabunge-wamchagua-cyril-ramaphosa-kuwa-rais-afrika-kusini-kwa-awamu-pili-44-rickmedia

 Mjumbe wa Chama Tawala cha African National Congress (ANC), Cyril Ramaphosa amechaguliwa tena na Wabunge kuwa Rais wa Taifa hilo kwa Awamu ya Pili akipata kura 283 na kumshinda Kiongozi wa chama cha EFF, Julius Malema aliyepata Kura 44

Licha ya ushindi huo, Ramaphosa anakwenda kuongoza Serikali iliyoundwa chini ya Umoja wa Kitaifa ikiwa ni baada ya ANC kushindwa kufikisha 40% ya Kura zilizopigwa katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Mei 29, 2024

Kwa hatua hiyo sasa, ANC inaungana na chama cha Democratic Alliance (DA) kwaajili ya kuunda Serikali mpya ikiwemo kushirikiana katika uteuzi wa Viongozi wa nafasi mbalimbali za Kiutawala