Mjumbe wa Chama Tawala cha African National Congress (ANC), Cyril Ramaphosa amechaguliwa tena na Wabunge kuwa Rais wa Taifa hilo kwa Awamu ya Pili akipata kura 283 na kumshinda Kiongozi wa chama cha EFF, Julius Malema aliyepata Kura 44
Licha ya ushindi huo, Ramaphosa anakwenda kuongoza Serikali iliyoundwa chini ya Umoja wa Kitaifa ikiwa ni baada ya ANC kushindwa kufikisha 40% ya Kura zilizopigwa katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Mei 29, 2024
Kwa hatua hiyo sasa, ANC inaungana na chama cha Democratic Alliance (DA) kwaajili ya kuunda Serikali mpya ikiwemo kushirikiana katika uteuzi wa Viongozi wa nafasi mbalimbali za Kiutawala