Universal Music yatangaza kufanya kazi na Lady Jay Dee rasmi

-rickmedia: Saraphina Jerry

Saraphina Jerry

1 hour ago
rickmedia: universal-music-yatangaza-kufanya-kazi-lady-jay-dee-rasmi-782-rickmedia

Universal Music Group (UMG), moja ya lebo kubwa zaidi za muziki duniani, imetangaza rasmi ushirikiano na msanii nguli wa Tanzania Lady Jaydee kupitia tawi lake la Afrika Mashariki.

Kupitia Universal Music Group East Africa, UMG imeeleza kujivunia kushirikiana na Lady Jaydee, msanii ambaye amekuwa na mchango mkubwa na wa kudumu katika muziki wa Afrika Mashariki. Kazi zake zimeendelea kugusa vizazi mbalimbali kutokana na ujumbe mzito na ubora wa hali ya juu.

Ushirikiano huu unaakisi imani ya pamoja katika nguvu ya muziki wa Afrika Mashariki na dhamira ya kuupeleka katika jukwaa la kimataifa. Pia ni hatua muhimu katika kuinua vipaji na sauti zenye heshima kutoka ukanda huu.

UMG imeeleza kuwa kupitia ushirikiano huo, wanakusudia kukuza ubunifu, kupanua wigo wa muziki wa Afrika Mashariki duniani, pamoja na kujenga urithi imara kwa kizazi cha sasa na kijacho, wakisisitiza kuwa huu ni mwanzo wa safari mpya yenye mafanikio makubwa.